Sunday 8 June 2014

DEWJI AWAITA WAANDISHI AZUNGUMZE KUHUSU MALINZI, WAMBURA

DEWJI (KATIKA) AKIWA NA KOCHA WA ZAMANI WA SIMBA, MILOVAN CIRKOVIC (KULIA), MWINGINE NI MWANACHAMA WA SIMBA
Mfadhili wa zamani wa Simba, Azim Dewji amewaita waandishi wa habari.
Ingawa bado hajaweka wazi anataka kuzungumzia nini, lakini SALEHJEMBE imeng’amua Dewji anataka kuzungumzia suala linalohusu mgombea wa urais aliyeengulia baada ya kugundulika uanachana wake una walakini, Michael Wambura na Rais wa TFF, Jamal Malinzi.
“Kweli Dewji atakuwa na kikao saa 5 asubuhi, nafikiri ana kitu kuhusiana na Wambura na Malinzi.
“Lakini sijajua ni nini hasa, lakini Dewji atazungumza mwenyewe Jumapili, vizuri ukaenda na kujua,” alisema mpasha habari.
Tayari Wambura amekata rufaa TFF kupinga kuondolewa kwenye uchaguzi na kamati ya uchaguzi ya Dkt Damas Daniel Ndumbaro.
CHANZO; Saleh Ally blog

No comments:

Post a Comment