Tuesday 10 June 2014

NEYMAR AUMIA BRAZIL WAKIWA MAZOEZINI

 Mshambuliaji nyota wa Brazil, Neymar jana aliumia mazoezini na kuzua hofu kubwa.
Wabrazil ndiyo wanamuweka mbele kama tegemeo namba moja, Neymar aliumia enka na baada ya muda aliweza kuendelea na mazoezi lakini baada ya kupatiwa tiba kwa muda kadhaa.
Hali hiyo imezua hofu kama kweli Neymar atakuwa katika kiwango safi katika mechi ya ufunguzi dhidi ya Croatia.
Neymar ndiye nyota ambaye Brazil wanaamini atakuwa shujaa wao katika michuano ya Kombe la Dunia inayoanza keshokutwa.
Lakini hakuna taarifa yoyote kutoka kwenye kikosi hicho iliyosema anaweza asiwe katika kiwango kizuri.

No comments:

Post a Comment