Wednesday 29 April 2015

Yanga kukabidhiwa kombe mbele ya Azam

KLABU ya Yanga inatarajiwa kukabidhiwa kombe lake la ubingwa wa Ligi ya Vodacom Tanzania bara Mei 6 kwenye uwanja wa taifa Dar es Salaam
KLABU ya Yanga inatarajiwa kukabidhiwa kombe lake la ubingwa wa Ligi ya Vodacom Tanzania bara Mei 6 kwenye uwanja wa taifa Dar es Salaam baada ya kumalizika pambano kati yao na waliokuwa mabingwa watetezi Azam FC.
Waziri wa michezo Dr Fennela Mkangara ndiye atakaye kabidhi kombe hilo la 25 kwa mabingwao hao wa Kihistoria baada ya jana jumatatu kuifunga Polisi Moro mabao 4-1, na kufikisha pointi 55 ambazo hazitaweza kufikiwa na timu nyingine inayoshiriki ligi hiyo msimu huu.
Rais wa Shirikisho la soka Tanzania TFF, Jamal Malinzi ameiambia Goal siku hiyo itakuwa rasmi kukabidhi baadhi ya zawadi kwa washindi wa ligi hiyo na ndiyo sababu wakamteuwa waziri kuwa mgeni rasmi.
“Kwanza nampongeza Mwenyekiti wa klabu ya, Yusuf Manji kwa timu yake kutwaa Ubingwa wa Ligi ya Vodacom msimu wa 2014/2015 , kwasababusiyo kazi nyepesi na jambo muhimu sasa wanapaswa kuanza maaandalizi kwa ajili ya michuano ya kimataifa barani Afrika mwakani.

No comments:

Post a Comment