Monday 13 April 2015

ULIMISS MATOKEO YA BARCLEONA LEGENGS VS TANZANIA LEGENDS? BARCELEONA LEGENDS BEAT TANZANIA LEGENDS 2-1

TIMU ya wachezaji wakongwe wa Barcelona imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wakongwe wa Tanzania ‘Tanzania Stars katika mchezo wakirafiki wa kimataifa uliofanyika kwenye uwanja wa taifa Dar es Salaam.
Mshambuliajia Luis Garcia ndiye aliyekuwa wa kwanza kuifungia bao la kuongoza Barcelona dakika ya tisa baada ya kuunganisha kwa kichwa krosi ya Kluivert na kumwacha kipa Peter Manyika akiusindikiza kwa macho mpira.
Wakongwe wa Tanzania Stars walijitahidi kufanya mashambulizi kwenye lango la Barcelona na dakika ya 44 Yusufu Macho aliisawazishia timu yake bao hilo kwa shuti kali baada ya kuunganisha mpira uliokuwa umeokolewa na mabeki wa Barcelona.
Hadi mapumziko timu hizo zilikuwa sare ya 1-1 huku wageni Barcelona wakiutawala zaidi mchezo huo kwa kufanya mashambulizi mengi.
Kipindi cha pili Barcelona, walikianza kwa kasi na kufanya mashambulizi mfululizo kwenye lango la Tanzania Stars na washambuliaji wake Simao Sambrosa na Luis Garcia wakapoteza nafasi nyingi walizozipata.

Mchezo huo uliendelea kuwa wa kasi na ushindani mkubwa kwa pande zote mbili kutafuta bao la ushindi lakini walikuwa ni Barcelona waliofanikiwa kushinda kombe hilo baada ya Patrick Kluivert kufunga bao la pili kwa penati dakika ya 86. kufuatia Sambrosa kuangusha kwenye eneo la hatari na Mustapha Hoza ambaye katika mchezo huo alionyesha kiwango cha juu.
Wachezaji wa Tanzania Stars kama Mohamed Hussein Madaraka Seleman, Edibili Lunyamila na Dua Said na Bakari Maliwa walijitahidi kuonyesha uwezo wao wa kupambana na wenzao wa Barcelona lakini walishindwa kusawazisha bao hilo.
Hiyo nimara ya pili kwa Tanzania Stars kupoteza mchezo wa kimataifa wa kirafiki kwani Agosti 28 2014 walicheza na timu ya wakongwe wa Real Madrid na kufungwa mabao 3-1 kwenye uwanja huo wa taifa Dar es Salaam Tanzania.

No comments:

Post a Comment