Tuesday 17 March 2015

Match Preview: Yanga - Kagera Sugar, Yanga kulipa kisasi

Mbali na kutaka kulipa kisasi lakini pia Yanga ambao ni wawakilishi pekee kwenye michuano ya kimataifa watataka kushinda mchezo huo ili kurudi kileleni mwa ligi kuu
MABINGWA mara 24 wa Ligi ya Vodacom Tanzania bara Yanga kesho Jumatano watashuka kwenye uwanja wa taifa Dar es Salaam kuwaalika Kagera Sugar ya Bukoba.
Yanga inayoshika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 31, itaingia kwenye mchezo huo ikiwa na lengo la kulipa kisasi cha kufungwa bao 1-0, na Kagera katika mchezo wa awamu ya kwanza uliofanyika kwenye dimba la Kaitaba Novemba 2014.
Mbali na kutaka kulipa kisasi lakini pia Yanga ambao ni wawakilishi pekee kwenye michuano ya kimataifa watataka kushinda mchezo huo ili kurudi kileleni mwa ligi hiyo baada ya kuzidiwa na wapinzani wao Azam kwa pointi mbili lakini wakiwa nyuma kwa mchezo mmoja.
Kabla ya kufungwa na Simba wiki mbili zilizopita kikosi cha Yanga kiweza kushinda mechi tatu mfululizo kikiwa ugenini kwenye viwanja wa vya Mkwakwani Tanga walipoifunga Coastal Union na kisha kuchukua pointi sita kwenye uwanja wa sokoine Mbeya kwa kuzifunga Tanzania Prisons na Mbeya City.

Pamoja na kuvurugiwa na Simba kwa kufungwa bao 1-0 Machi 8, niwazi Yanga wataingia kwa kasi kutaka kuifunga Kagera Sugar na kurudisha heshima yao ikiwemo kuendeleza furaha iliyowapa mashabiki wake wikiendi iliyopita kwa kuifunga FC Platinum ya Zimbabwe mabao 5-1, ukiwa ni mchezo wa kombe la Shirikisho Afrika CAF.
Kocha Hans van der Pluijm, hakuwepo kwenye timu wakati timu yake inafungwa bao 1-0 na Kageral lakini kurejea kwake kwenye kikosi cha Yanga niwazi kumeonyesha mabadiliko na atahakikisha vijana wake wanapambana kupata pointi tatu ili kujipa matumaini ya kufanya vizuri kwenye mechi zijazo.
Pluijm ameiambia Goal anaiheshumu Kagera Sugar inayonolewa na kocha Mganda Jackson Mayanja, lakini akasema pamoja na heshima hiyo amekiagiza kikosi chake pointi tatu katika mchezo huo ili kuweka mazingira mazuri ya ubinga.
“Tupo katika ari ya juu kuhakikisha tunaendeleza wimbi la ushindi tulioupata Jumapili kwenye mchezo dhidi ya FC Platinum, najua Kagera ni timu nzuri iliwafunga Simba uwanja wa taifa lakini tumejiandaa kuhakikisha tunapambana na kupata ushindi kabla ya kwenda Tanga, amesema Pluijm.
Naye kocha Jackson Mayanja amesema anajitambia vijana wenye umri mdogo na viwango vya juu kwenye kikosi chake hivyo hatishiki anachojua amekuja Dar es Salaam kuchukua pointi tatu kama alivyofanya kwenye mchezo wa kwanza.
Kwenye msimamo wa ligi Kagera inashika nafasi ya nne ikiwa na pointi 25 na katika pambano lake lililopita dhidi ya Coastal Union ili ilazimisha sare ya 2-2.
“Tunamatumaini ya kuifunga Yanga tupo vizuri vijana wote wapo sawa na tunacho subiri ni muda wa mchezo ili tuweze kuchukua kilichotuleta Dar es Salaam ,”amesema Mayanja.

No comments:

Post a Comment