Na Augostino Mabalwe kwa msaada wa Mtandao
BAADA ya mkataba wake mwaka
2009 kumalizika katika klabu ya Manchester City, Daniel Sturridge
alitua katika klabu ya Chelsea na kusaini mkataba wa miaka minne katika
timu hiyo iliyokuwa chini ya kocha Carlo Ancelotti.
Sturridge alifunga goli lake la
kwanza katika klabu ya Chelsea katika mechi yake ya kwanza katika
ushindi wa 2-1 dhidi ya Seattle Sounders ikiwa ni mechi ya kirafiki
iliyopigwa tarehe 18 Julai 2009.
15 Septemba 2010 Daniel
Sturridge alifunga goli lake la kwanza katika michuano ya klabu bingwa
barani ulaya katika mchezo ambao Chelsea walicheza dhidi ya MSK Zullin
ikiwa ni mechi yake ya kwanza katika michuano hiyo.
Baada ya kucheza kwa takribani
misimu mitatu katika klabu ya Chelsea,Januari 2, 2013 Daniel Sturridge
alisajiliwa na klabu ya Liverpool kwa ada ya paundi milion 12.
Daniel Sturridge aliendeleza
rekodi yake ya kufunga katika mechi zake za kwanza katika timu na
michuano mbalimbali baada ya kufunga dakika ya 7 ya mchezo katika mechi
yake ya kwanza katika ushindi wa Liverpool wa 2-1 dhidi Mansfield Town
ukiwa ni mchezo wa kombe la FA mzunguko wa tatu uliopigwa Jan 6, 2013.
Mechi yake ya kwanza ya ligi
katika klabu hiyo ilikuwa ni dhidi ya Manchester United ambapo aliingia
kutokea benchi na kufunga goli lake la kwanza la ligi klabuni hapo licha
ya timu hiyo kufungwa 2-1 na mashetani wekundu katika mchezo huo
uliochezwa Jan 13 2013.
Sturridge alifunga goli lake la
pili la ligi katika mechi yake ya kwanza kuanza katika kikosi cha
kwanza cha Liverpool katika ushindi wa 5-0 dhidi ya Norwich Jan 19,
2013 mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Anfield na kufanya mchezaji huyo
kufunga magoli matatu katika mechi zake tatu za mwanzo hivyo kuwa
mchezaji wa kwanza wa Liverpool kufanya hivyo tangu Ray Kennedy
alipoweka rekodi hiyo mwaka 1974.
Msimu wa 2013/2014 aliweka
rekodi katika ligi kuu nchini uingereza ya kuwa mchezaji aliyefunga goli
la haraka zaidi katika mechi ya ufunguzi ya ligi katika msimu
huo,Sturridge aliweka rekodi hiyo baada kufunga goli katika mechi ya
ufunguzi ambayo Liverpool waliibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Stoke
City.
Pia katika msimu huu Daniel
Srurridge ameendeleza moto wake katika ligi baada ya kufunga katika
mechi ya ufunguzi ambayo majogoo hao waliibuka na ushindi 2-1 dhidi ya
Southampton mchezo uliopigwa katika uwanja wa Anfield na siku chache
baadaye mchezaji huyo aliumia wakati akiitumikia timu ya taifa ya
England.
Alirejea uwanjani katika mechi
dhidi Westham United 31, Jan 2015 na kufunga goli katika mechi hiyo
ukiwa ni mchezo wake wa kwanza tangu atoke majeruhi.
Leo liverpool itakuwa katika
uwanja wake wa nyumbani wa Anfield kuikaribisha Besiktas ya nchini
uturuki katika mchezo wa michuano ya europa na hii itakuwa mechi ya
kwanza ya Daniel Sturridge ya michuano ya ulaya katika klabu hiyo baada
ya hapo awali kukosa mechi za ligi ya mabingwa barani ulaya kutokana na
kusumbuliwa na maumivu ya mguu.
Macho yote ya mashabiki wa
Liverpool yataelekezwa kwa Daniel Sturridge kutokana na rekodi zake za
kufunga katika mechi zake za kwanza katika michuano mbalimbali
No comments:
Post a Comment