Friday 20 February 2015

AZAM YABANWA YANGA YAPAA KILELENI

Yanga imerejea kileleni Ligi Kuu Bara  baada ya kuichapa Prisons ya Mbeya kwa mabao 3-0.

Ushindi huo umeifanya Yanga kufikisha pointi 28 dhidi ya Azam FC yenye 26 ambayo imelazimishwa sare ya bila mabao dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa  Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.

Yanga imebuka na ushindi huo mnono kwenye Uwanja wa ugenini wa Sokoine jijini Mbeya ikiwa ni baada ya viungo wake Simon Msuva na Andrey Coutinho kufunga.

Msuva amepachika mabao mawili, huku Coutinho na kukamilisha idadi ya tatu bila dhidi ya kikosi cha David Mwamwaja ambaye alitamba leo ingekuwa kazi ngumu kwa Yanga.

Pamoja na kuwa ugenini, Yanga walitawala mchezo kwa vipindi vyote huku wakipoteza nafasi nyingi za kufunga.

Mara kadhaa, Prisons nao walijitutumua hata hivyo kwa dakika zote 90 walifanikiwa kufanya mashambulizi makali au makubwa matatu tu.

Kwa kipigo hicho, Prisons inaendelea kubaki mkiani ikiwa na pointi 11 hivyo kuwa katika wakati mgumu na hofu ya kuteremka daraja.


Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, Azam FC wamekubali kuipisha Yanga kileleni.


Azam FC imetoka sare ya bila kufungana dhidi ya Ruvu Shooting katika mechi iliyochezwa  kwenye Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi, Pwani.

Sare hiyo ya bila mabao, inaifanya Azam FC kufikisha pointi 26 wakati Yanga ambayo imeibuka na ushindi dhidi ya Prisons inafikisha pointi 28.

Azam FC ndiyo inaongoza kwa kuwa na pointi 25 sawa na Yanga lakini tofauti ilikuwa ni mabao ya kufunga na kufungwa.

Katika kipindi cha kwanza dakika 15 za kwanza, Azam FC ilishambulia zaidi, lakini washambuliaji wake John Bocco na Kipre Tchetche hawakuwa makini.

Kipindi cha pili, mambo yalibadilika na Ruvu Shooting kutawala huku wakionekana kuwasumbua Azam FC, hata hivyo nao hawakuwa makini kumalizia nafasi walizozipata.

No comments:

Post a Comment