Thursday 14 May 2015

Ndemla aikata maini Yanga, Asaini Mkataba Mpya

WAKATI Waganda Joseph Owino na Dan Sserunkuma wakiropoka yao baada ya kutemeshwa kazi Simba, kiungo mahiri wa klabu hiyo, Said Ndemla ameikata maini Yanga iliyokuwa inamnyatia kwa kumwaga wino mkataba wa miaka miwili.
Taarifa za ndani za Simba zinasema kuwa, Ndemla amesaini mkataba huo jana mchana na kulipwa kiasi cha Sh40 milioni pamoja na gari ili kumtuliza mzuka baada ya kuenea kwa habari kwamba Yanga walikuwa tayari kumalizana na mchezaji huyo chipukizi.
Inaelezwa kuwa Kamati ya Usajili ya Simba ililazimika kumaliza mambo mapema kwa kuhofia kuzidiwa ujanja na Yanga ambayo imekuwa ikimmezea mate kiungo huyo, ambaye tangu apatishwe katika kikosi cha wakubwa toka timu ya vijana amekuwa gumzo kwa soka lake.

No comments:

Post a Comment