Monday 15 June 2015

Amechangia ubingwa wa Yanga kwa asilimia 75 na mengine usiyoyajua kuhusu Simon Msuva

SIMONI Msuva ndiye mchezaji bora wa Ligi ya Vodacom Tanzania bara msimu wa 2014/15 lakini unamjua vizuri mshindi huyo wa tuzo mbili?
SIMONI Msuva ndiye mchezaji bora wa Ligi ya Vodacom Tanzania bara msimu wa 2014/15 lakini unamjua vizuri mshindi huyo wa tuzo mbili nyingine ikiwa ni ya ufungaji bora sehemu alizopitia hadi kufika hapo?
Msuva amechangia Ubingwa wa Yanga kwa Asilimia 75
Msuva aliyechangia asilimia 75 ya ubingwa wa Yanga msimu uliopita kwa mabao yake 17 pamoja na kutoa pasi za mwisho 12 ambazo zilizaa mabao
Aliwahi jaribu Bahati katika muziki
Amepitia mahangaiko mengi ikiwemo fani ya uchezaji muziki kabla ya kugeukia katika soka. Awali mwanzoni mwa miaka ya 2010 kinda huyo aliwahi kuwa ni mmoja wa vijana wanaojifundisha muziki kwenye kundi la kulea vipaji la Tanzania House of Talent THT, na kuonekana kwenye kumbi mbalimbali za burudani akiwa ni densa wakati wasanii wakubwa wa kundi hilo wakutoa burudani.
Lakini baada ya miaka kadhaa ya kukaa kwenye kundi hilo pasipo kupata mafanikio aliona nivyema akatafuta fani nyingine ambayo inaweza kumtoa kimaisha ndipo alipogeukia katika mchezo wa soka na moja kwa moja akajiunga kwenye kituo cha kukuza vipaji vya vijana wadogo kiitwacho Wakati Ujao.
Anaongoza kwa staili nyingi za kushangilia
Msuva anayeongoza kwa kuwa na staili nyingi za ushangiliaji pindi anapofunga magoli
Aliwahi kuchezea Azam
aliwahi kuchukuliwa na kituo cha kuleleza vijana cha Azam ambacho baadaye kilimuacha na mchezaji huyo akasajiliwa na timu ya Moro United ambayo hata hivyo haikudumu kwenye ligi ya Vodacom na mwishoni mwa msimu ilishuka na kuwa mchezaji huru.
Alisajiliwa na Yanga msimu wa 2011/12
Msimu uliofuata wa 2011/12 nyota huyo akasajiliwa na Yanga hapo ndipo mafanikio ya mchezaji huyo yalipoanza kuonekana kwa kuanza kufanya vizuri na kutengeneza nafasi nyingi za magoli kwa timu yake licha ya kuonyesha mapungufu kadhaa mwanzoni mwa msimu kwa kuwa mbinafsi na kushindwa kutengeneza nafasi kwa wenzake.

No comments:

Post a Comment